"Cheka Unenepe" Unaionaje Shule Hii?


Cheka kidogo upunguze stress, imagine mwanao au wewe mwenyewe ndo ingekuwa shule yako au
unatakiwa ukaifundishe kama ticha? Majina ya Hizi shule nyingine kaazi kweli kweli!!!



Diva wa Clouds FM, Atupia Picha za Mapaja yake Instagram



Mtangazaji wa Ala za Roho, kupitia Clouds FM, Loveness Love au Diva, naye ameachia picha za Utata akionesha ni kiasi Mungu kamjaalia hasa upande wa Mapaja, Kupitia Akaunti yake ya Instagram amezitupia picha hizo na kuwaachia mashabiki waseme wenyewe. Vp wewe mshabiki wangu wamwonaje?

Sio kila siku tu anamwelezea Prezoo, Leo kaweka Paja anawaskilizia wadau mna lipi la kusema.
Picha hizo zikielea ndani ya Instagram

Nick Minaj Atupia Picha ya Utata Instagram, azidi kumtesa Dj Khaled.



Mwanamuziki Nick Minaj, 30, amechia picha nyingine yenye utata katika Instagram, huku ikiwa imezificha sehemu za chuchu tu za Maziwa yake. Mbali na hayo msanii huyo alizidi kumtupa Dj Khaled ambaye wiki chache zukizopita alijitoa katika TV na Kumchumbia Rasmi, Tukio Lililo washangaza wengi.



Nick alisema kwamba Khaled ni Kaka yangu na hakuwa Serious na kile alichokifanya, acheni jamani alikuwa anatania tu, ilikuwa ni mbinu tu ya kujitangaza na Khaled anipendi kihivyo, wala hajawahi kuvutiwa na mimi.


Lol!! Wafany* mapenz* Juu ya Ghorofa Bovu



Picha hiyo iliweza kupigwa na Mfanyakazi mmoja aliyekuwa karibu na jengo hilo ambalo juu yake kulikuwa na watu wawili wakiendelea kufanya mapenzi kwa raha zao.

Jengo hilo la kihistoria lipo Huko New Castle maarufu kama " New Castlen Ancient City Walls" Lilijengwa mnamo karne za 14 na 15 kama kinga ya kuwazuia wavamizi wa Scottland.


Baada ya Mfanyakazi huyo, Solomon Gallagher kuwapiga hiyo picha akaiweka Twitter na kisha kusema:-
"Congratulations to the happy couple who just had $*x on top of the Newcastle city wall. Rumbled," 

Diamond Coca Boy, Now Meet Rihanna AK 47 Girl.



Pop Star, Rihanna ameweka Picha hii katika Instagram akionesha jinsi gani ameweka jino la Dhahabu lenye Taswira ya Bunduki aina ya AK 47. You cant even imagine the cost of the Teeth.


"Niite Tena Boss Mfupi Uone Ntakufanya Nini" Aki



Muigizaji Kutoka Nchini Nigeria, Chinedu Ikedieze, maarufu kama Aki, amewatahadharisha mashabiki wake wanaomfuata kupitia twitter kamwe wasimuite "BOSS MFUPI" kwasababu anachukizwa na jina hilo, na badala yake wamuite The Boss tu au vinginevyo atawa block wasiwasiweze kuwasiliana tena.

Aki ambaye aliwika sana kipindi cha Movies za " Aki na Ukwa", si mtoto tena, kwani ameshaoa Tangu mwaka 2011, na Mwanamke Huyo Hapo Juu katika picha.

Wow!! Angalia Beyonce Alivyotokelezea Kichwani Baada ya Kunasa Nywele katika Feni akiwa Katika Show!!!


Msanii wa R&B, Beyonce ameamua kubadilisha muonekano wa Nywele zake na kuzifupisha kidogo baada ya tukio la kunasa katika Feni alipokuwa akifanya Show ya "Halo" huko Montreal.

Tukio lililowafanya wasaidizi wake na Crew Members kuwahi kuzima feni hilo na kuzitoa nywele hizo huku mwenyewe akiendea Kuimba bila kupote na beat, Naiman sas hakinasi kitu.

Polisi Mlevi Auwa1, na Kujeruhi 3 kwa Risasi Akiwemo Mjamzito.



Koplo Mohamed Abubakar wa MOPOL 17, Akure, Jimbo la Ondo katika Mji wa Festac anasakwa na Polisi baada ya Kuuwa Raia Mmoja na Kuwajeruhi Raia wengine watatu na Mama Mjamzito mmoja kwa kutumia silaha.

Walioshuhudia tukio hilo wamesema yalizuka mabishano kati ya baadhi ya Raia hao na Askari katika Mgahawa mmoja wa Chakula Mjini hapo, baada ya Askari huyo kupandwa na hasira alichukua silaha hiyo na kuwafyatulia Risasi Raia hao na kisha kutoroka eneo hilo.

Majeruhi wengine wanaendelea vizuri akiwemo mjamzito huyo na wataruhusiwa kwenda nyumbani hivi karibuni ingawa mmoja wao anhitaji afanyiwe Upasuaji.

Kamanda wa Polisi wa Jimbo Hilo Bw. Umar Manko amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na ameshangazwa na kitendo cha askari huyo wa Gari kutoka kitongoji cha Akure Kuwa Lagos Muda huo na Mpaka akafanya mauji na kujeruhi Raia Hao.

Juhudi za Kumsaka Koplo huyo zinaendelea.

Msanii wa Filamu Hajakutana na Mwanaume Miaka 2, anahitaji Mwanaume wa Kweli.


Msanii wa Nolly Wood, Karen Igho ameandika kupitia Ukurasa wake wa Twitter ya Kwamba hajakutana na mwanaume kwa kipindi cha Miaka miwili sasa kwani anahitaji Mwanaume wa kweli wa kumuoa, Hii imetokana na wimbi la wanaume wa huko kuwakimbilia wasanii kwa lengo la wao kujipatia umaarufu na kuwabwaga, huku kukizidi kuongezeka uvunjifu wa ndoa za Mastaa kwao kila leo.

Diamond Ala Shavu la Kutangaza Coca cola, Angalia Picha za Uandaaji wa Tangazo Hilo.





Hizo ni Baadhi ya Picha Ambazo Msanii Diamond Platnumz Aliziweka katika Instsgram yako akionesha jinsi hali ilivyokuwa katika utengenezaji wa Tangazo la Soda ya Cocacola Huko South Africa.



Diamond Alikuwa Miongoni mwa Abiria waliokwama jana kutokana na ajali ya moto katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta, na aliendelea na Safari baada ya kukodiwa Ndege Binafsi na Coca Cola.

Raia Wawili wa Uingereza Wamwagiwa Tindikali Zanzibar.

Majeruhi wa Tindikali, Si wa Habari Hii
Raia wa kigeni kutoka katika nchi ya Uingereza ambao wanafanya kazi ya kujitolea katika upande wa Ualim   wamemwagiwa tindi kali mjini Zanzibar jana  mida ya saa moja usiku katika mitaa ya shangani mji mkongwe  Zanzibar habari kutoka katika chanzo chetu cha habari  kinasema jeshi la polisi zanzibar limeanza msako na kuwatafuta watu waliofanya kitendo hicho.

  walimu hao ambao wamefika mjini Zanzibar kwa kujitolea kufundisha walitambulika kwa majina ya Kate Gee miaka 18 na kirsiwer Trup pia miaka 18 walimu hao wa kujitolea wanatoka katika nchi ya Uingereza (UK)  raia hao wameingia kisiwani hapo takribani wiki mbili tu na kukutwa na majanga hayo ambao walikuwa wanafanya kazi katika shule  moja ya msingi inayojulikana kama Mtakatifu Monika iliyopo chini ya kanisa la Aglicana. habari tulizozipata hivi punde  Raia hao hivi sasa wamehamishiwa katika Hospitali ya Aghakani jijini Dar es salaam kwa matibabu zaid tutazidi kuwaleta habari zaidi

From: Swahilitz

MCHINA, Amteka Binti na Kumfunga Minyororo Kisha Kumbaka Kwa Siku 11 Mfululizo Chumbani Kwake.

ion.com/pagead/show_ads.js" type="text/javascript">
Mwanaume mmoja Anashikiliwa na Polisi kwa Kosa la kumteka nyara na kumbaka kwa siku 11 mfululizo binti wa miaka 18, ambaye alimfungia ndani ya jela aliyoijenga chini ya chumba alichokuwa akiishi.

Chen Xiaolong, 36, Mkazi wa Jimbo la Jiaxing, Zhejiang, China, alikiri kutenda makosa hayo baada ya kukamatwa na polisi kufuatia kutoroka kwa msichana huyo. Chen ambaye alikuwa akimtishia kwa kisu kila siku na kumbaka binti huyo kwa zaidi ya siku 11, alipata hamasa ya kufanya ukatili huo baada ya kuangalia picha za ngono na kupitia mtandaoni.


Msichana huyo aliweza kujinasua kutaka katika minyororo kupitia Mashine ndogo ya kukatia kucha na ndipo akasogea juu na kupiga kelele za kuomba msaada kwa majirani huku akiwasihi wamuokoe maana akirudi atamuua.

Polisi walikuta Kiji chumba kidogo uvunguni ambako Cheni alikijenga na kukizungushia Magazeti na Carpets ambako ndipo alipokuwa akimfanyia binti huyo Unyama huo.

Gereza ambalo alikuwa anafungiwa Binti Huyo
SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days
Alikuwa anaruhusiwa kuja juu mara mbili tu kwa ajili ya kuoga na kisha humrudisha gerezani
SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days

SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days
Alikutana nae Bar, Akamshawishi waende nyumbani, alipofika alimtolea kisu na kumtishia kumuua, hapo ndipo alipofanikiwa kumvua nguo zote na kumfunga Minyororo na kisha kumficha katika chumba chake hicho ambacho hakikuwa kinajulikana.

SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days

SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days
Pia alimtishia kuziweka picha zake za Utupu Mtandaoni ikiwa angembishia matakwa yake
SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days
Kitambulisho cha Chen
SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days
Geto kwa Chen
SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days
Taswira ya Nyumba hiyo kwa Nje
SEX HOSTAGE: Woman, 18, Kept In Underground Cell For 11 Days
Majirani wakiwa nje, baada ya msichana huyo kuokolewa
READ MORE: http://news.naij.com/42896.html

Mume wa Pili wa Wastara Aibuka na Kuzua Mapya


Na Issa Mnally
MIEZI nane baada ya kufariki dunia mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’, hatimaye mume wa pili wa staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma aitwaye Ahmed Kushi ameibuka na kudai kwamba anatambua kwamba staa huyo bado ni mkewe na anataka ampatie mwanaye aliyezaa naye.
Ahmed Kushi na Wastara siku ya ndoa yao.
Kwa muda mrefu kulikuwa na taarifa kuwa Wastara aliachana na mwanaume huyo kwa talaka kabla ya kuolewa na Sajuki lakini kuibuka kwake na madai kuwa bado mwanadada huyo ni mkewe kumezua mshangao mkubwa.
MADAI YA KUSHI
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Kushi alifunguka kwa mara ya kwanza kuwa yeye na Wastara walifunga ndoa ya Kiislamu mwaka 2000 na kujaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume aitwaye Fares.
Alisema: “Kisheria bado ni mke wangu kwa kuwa nilikuwa nimempa talaka moja tu wala hazikufika tatu,” alisema Kushi na kudai kwamba ndoa yake na staa huyo ilidumu kwa mwaka mmoja na nusu na kuvunjika kutokana na kutawaliwa na migororo.
Jamaa huyo alidai kuwa zaidi ya mara tatu amekuwa akimtaka Wastara ampatie mwanaye huyo ambaye kwa sasa ametimiza miaka minane bila ya mafanikio.
KWA NINI WAKATI HUU?
Gazeti hili liliamua kumbana kwa kumuuliza kwa nini ameibuka wakati huu baada ya Sajuki kufa na mbona hakujitokeza kwa zaidi ya kipindi cha miaka kumi iliyopita? Pia akaulizwa kwa nini ameamua kutafuta umaarufu kwa kumdhalilisha? Akaishia kukaa kimya.

WASTARA AFUNGUKA
Baada ya Kushi kuibuka na ishu hiyo yenye utata, gazeti hili lilizungumza na Wastara ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Kuhusu mtoto, kama kweli alikuwa na lengo la kumchukua mwanaye na ananijua, basi atakuwa anawajua wazazi wangu hivyo angefuata utaratibu.
“Hakuna utaratibu kama huo kama kweli anamhitaji mwanaye angeenda kwa wazazi wangu, huko ni kunidhalilisha kwa kuwa ananiona mnyonge baada ya kufiwa na mume wangu Sajuki.
“Kama siyo kunidhalilisha ni nini? Naomba asitumie jina langu kutafuta umaarufu kwa kunichafua. Naomba aache kwa sababu ananiongezea maumivu juu ya maumivu.”
Kuhusu madai kwamba bado ni mkewe, Wastara alilia: “Hivi huyo mtu alikuwa wapi muda wote nikiwa na Sajuki? Mbona hakuibuka wakati mume wangu akiwa hai? Najua anatumia kigezo cha kuondoka Sajuki kunionea lakini Mungu anajua.”
NI KWELI ALIFUNGA  NDOA NA KUSHI?
Pamoja na kumbembeleza aeleze kama kweli aliwahi kufunga ndoa na Kushi, Wastara alisema: “Sitaki kumzungumzia mtu, naomba watu wawe na huruma kwangu, wasitumie kigezo cha kumpoteza Sajuki kunidhalilisha.”

SHEHE AMPINGA KUSHI
Gazeti hili halikuishia hapo, lilimtafuta shehe wa Msikiti wa Nuur wa Magomeni-Mapipa jijini Dar, Juma  Simba ili kupata ufafanuzi juu ya talaka moja ambapo alimpinga Kushi kwa kusema kuwa kisheria Wastara si mkewe tena.
“Kumpa talaka moja si sababu ya kuendelea kuwa mke wake mpaka leo hii, sheria inasema kuwa Kushi alitakiwa kumrejea Wastara kabla ya miezi mitatu kupita tangu alipompa talaka moja,” alisema na kusisitiza kuwa ndoa hiyo ilishakufa.

YATOKANAYO
Awali ilidaiwa kuwa Wastara aliwahi kuolewa mara mbili kabla ya kufunga ndoa na staa mwenzake wa filamu, Sajuki.
Ndoa ya kwanza ya Wastara aliifunga mwaka 1998 na Juma Mpemba ambaye alibahatika kupata naye mtoto mmoja wa kiume aitwaye Samir.
Sajuki alikuwa mume wa tatu kwa Wastara ambaye naye alibahatika kupata mtoto mmoja wa kike aitwaye Farheen.

source: GPL

Mke Mtarajiwa Anaswa Akijiuza, Atupwa Gerezani hadi Agosti 20


ZA mwizi arobaini! Kauli hiyo ya wahenga ilitimia Jumatatu iliyopita kufuatia msichana Pili Baraka (21) aliyevishwa pete ya uchumba na mpenzi wake hivi karibuni (jina tunalihifadhi) kujikuta akitupwa Gereza la Segerea jijini Dar baada ya kunaswa kwa tuhuma za ukahaba, Amani linakupasha.
Mrembo huyo alifikishwa kwenye Mahakama ya Sokoine Drive (Jiji) na kusomewa shitaka na mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo, Richard Magodi mbele ya Hakimu Timothy Lyon.
Akisoma shitaka hilo, Magodi alisema: Agosti 5, mwaka huu, saa nane usiku, Pili alinaswa kwenye maeneo ya Manzese jijini Dar akifanya biashara ya ukahaba.
Aliposomewa shitaka lake hilo, Pili aliinamisha kichwa na kujibu kwa kifupi: Si kweli.
Licha ya kukana shitaka hilo, Hakimu Lyon alimtaka mchumba huyo wa mtu kutafuta wadhamini wawili lakini aligonga mwamba na kupelekwa Gereza la Segerea mpaka Agosti 20, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
Akijitetea kabla ya kupandishwa kwenye karandinga kwenda Segerea, Pili aliiomba mahakama hiyo imuonee huruma asiende kuilia Sikukuu ya Idd, Segerea kwa kuwa mchumba’ake yuko safarini kikazi na hakuwa na mtu mwingine wa kumwekea dhamana, ombi ambalo lilikataliwa.
Source: GPL

Mfanya Biashara wa Madini Auwa Kwa Kupigwa Risasi zaidi ya 6, Moshi


 Mfanyabiashara tajiri wa Mirerani na Jijini Arusha, Erasto Msuya, ameuawa kwa kupigwa risasi zaidi ya 20 kwa kutumia bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG), jana mchana.
Erasto anayemiliki vitega uchumi kadhaa na anayeaminika kuwa miongoni mwa wafanyabiashara wa Mirerani wanaoongoza kwa utajiri,
aliuawa jana saa 7:00 mchana wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.
“Eneo la tukio kumeokotwa maganda karibu 21 ya risasi zinazoaminika ni za SMG, yaani mwili ni matobo kila sehemu kwa kweli ameuawa kinyama sana,” alisema polisi mmoja wa Kituo cha Bomang’ombe.
Kufuatia mauaji hayo yaliyotokea kati ya neo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) na mji wa Bomang’ombe, mji huo ulifurika magari ya wachimbaji kutoka Moshi, Arusha na Mererani.
Habari za uhakika zilieleza kuwa wauaji wake walikuwa katika pikipiki na baada ya kumminia risasi hizo, walimpora kibegi ambacho haikujulikana kama kilikuwa na madini ama mamilioni ya fedha.
Kulingana na vyanzo vya habari, mfanyabiashara huyo alipigiwa simu na kukubaliana kukutana katikati ya mji wa Bomang’ombe na makutano ya Barabara ya Kia katika Barabara Kuu ya Hai kwenda Arusha.
RPC Kilimanjaro afafanua alivyouawa
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema kuwa mfanyabiashara huyo aliuawa saa 7:00 mchana eneo la Mjohoroni kati ya mji wa Bomang’ombe na makutano ya barabara ya Kia.
“Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa Eransto alikuwa akitokea Moshi kuelekea Arusha, na alipofika hilo eneo la Mjohoroni alichepuka na kwenda meta 300 nje ya barabara,” alisema.
Kamanda Boaz alisema alipofika eneo hilo, alikutana na vijana wawili waliokuwa na pikipiki ambao waliingia ndani ya gari kwa lengo la kufanya mazungumzo yanayodhaniwa ni ya kibiashara.
Hata hivyo, muda mfupi tu Erasto alishuka kwenye gari lake na kuanza kukimbia na ndipo mmoja kati ya wale vijana alishuka kwenye gari la Erasto na kuanza kumminia risasi nyingi.

Kijana wa Kimasai alivyoshuhudia mauaji Kijana pekee wa kabila la kimasai anayedaiwa kushuhudia mauaji hayo, aliwaeleza polisi kuwa mara baada ya Erasto kufika eneo hilo la mtaa wa Wasomali, alisimamisha gari na kuwapigia wauaji. Habari hizo zimedai kuwa vijana wale wawili walipokea simu hiyo na kumtaka ashuke kwenye gari lake la kifahari aina ya Range Rover New Model, ili wafanye biashara ambayo haijui.

 Inadaiwa kuwa Erasto alipojaribu kupeleka mkono ili achomoe bastola, mmoja wa wale vijana alianza kumshambulia kwa risasi nyingi ambazo zilimfanya afariki dunia papo hapo. Kijana huyo wa kimasai anayedaiwa kuwa msaada mkubwa kwa polisi, alidai kuwa baada ya Erasto kudondoka chini, vijana hao walichukua begi alilokuwa nalo na kutokomea.

 Pikipiki iliyotumika yapatikana.
     Taarifa zilizopatikana baadaye jana jioni zilisema pikipiki iliyotumika katika tukio hilo imepatikana katika kijiji cha Olkolili, huko Sanyajuu wilayani Siha mkoani Kilimanjaro. Kamanda Boaz alithibitisha kupatikana kwa pikipiki hiyo yenye nambari za usajili T316 CLV ikiwa imetelekezwa baada ya gurudumu moja kupata pancha baada ya kufika katika eneo hilo. “Kwa vile tulikuwa tumesambaza taarifa kila mahali kwamba kuna raia wema walituarifu kuwa kuna watu wametelekeza pikipiki, baada ya kupata pancha na walikuwa wakitembea kwa miguu,” alisema.

 Alisema Polisi walikwenda katika eneo hilo na mashuhuda walioshuhudia tukio hilo la mauaji wameitambua pikipiki hiyo kuwa ndiyo iliyokuwa ikitumiwa na wauaji wa mfanyabiashara huyo. Kamanda Boaz alisema pia kuwa polisi watachunguza kwa kina mawasiliano ya simu ya mfanyabiashara huyo, kwa lengo la kutafuta watu wa mwisho kuwasiliana na marehemu.

Source: Mwananchi

Angalia jinsi Natural Afro ilivyotunzwa mpaka kumfanya Apewe Tuzo ya maajabu Guiness.


Aevin Dugas, 38, Mfanyakazi katika Taasisi moja ya kijamii huko Louisiana anashikilia Rekodi ya Maajabu ya Guinness kwa kuwa na Nywele Nyingi za Kiasili (Afro) ambazo ki mzunguko zina urefu wa Futi 4 na Inchi 4.



Nywele hizo zimekuwa zikitunzwa kwa zaidi ya miak 14 mpaka kufikia zilipo, Ingawa anajivunia kuwa nazo lakini amekiri kuna wakati huwa ni usumbufu kwake na mzigo kwani kuna baadhi ya watu huwa hawaamini ni zake mpake wamshike nyele hizo.




Tangu Apate Tuzo Hiyo amekuwa ni Muongozo kwa wanawake hasa weusi kuachana na mambo ya Relaxers na dawa nyingine, badala yake waende Naturally.




Chris Brown Aamua Kustaafu Kuimba, Ni kutokana na Kuandamwa na Maskendo na Mabalaa


Mwanamuzi wa RnB wa Marekani, Chris Brown huenda akastaafu rasmi kuimba kutokana na kuchoshwa na kuandamwa na skendo na mabalaa. Msanii huyo amesema hayo kupitia Twitter na Akaachia Hizo Tweets Mbili.

Taarifa Kuhusu Moto Unaoendelea Kuwaka Katika Uwanja Wa Ndege wa Jomo Kenyatta Huko Kenya




Timu ya Dharula na Uokoaji Nchini Kenya Imefanya kazi kubwa ya Kuwahamisha Wasafiri na Raia kutoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta kufuatia kuzuka kwa moto Mkubwa Kuanzia Alfajiri ya Leo.



Moto Huo Ulianza majira ya Saa Kumi Alfajiri (04:30 A.m) Umeliathiri sana Jengo la Idara ya Uhamiaji Ingawa hakuna madhara kwa Binadamu yaliyotokea.

Afisa kutoka Jumuiya ya Msalaba Mwekundu wa Kenya Daniel Mutinda Alizungumza na Vyombo vya Habari na Kusema ya Kwamba " Mpaka sasa hatujajua nini hasa kimesababisha moto huu ambao ulianzia maeneo ya watu wanapofikia, Ingawa hakuna madhara Kwa Binadamu lakini Vikosi vyetu vinaendelea na Kupambana na Moto Huo"




Serikali kupitia Idara zake Mbali mbali zinafanya mawasiliano kuhakikisha Abiria wanofika na watakao fika wanaenda kutua kwa dharula katika viwanja vingine vya ndege Hususan Mombasa International Airport (Mombasa) na Eldoret International Air Port.

Ambaka Rafiki Yake Kisha kumpiga Picha za Uch na Kuziweka katika Mitandao ya Kijamii.


Awali ya yote Tunampa pole Thelma Lawrance, Msichana wa miaka 23, mwanafunzi kutoka Chuo cha Masuala ya Kiteknolojia kwa mkasa uliompata baada ya Kubakwa na Rafiki wake wa kawaida alipokwenda kuchukua " Memory Card" yake.

Thelma, Alifanyiwa unyama huo na Henry Aiyenero, 27, ambaye siku zote alikuwa akimchukulia kama rafiki yake wa kawaida ingawa kwa mara kadhaa alikuwa akimtongoza na kumshawishi kuhusu kufanya mapenzi lakini akawa anakataliwa.

Siku ya Tukio Thelma alikwenda kuchukua Memory card hiyo kwa Henry, alipofika Henry aliwahi kuufunga mlango, kisha akamtolea kisu na kumwambia aidha kubali Kupigwa Picha za Uch kupitia simu ya mwanaume huyo au ampe "Penzi"

Thelma alikubali kuvua nguo na kumwambia atampa Penzi lakini asimpige Picha, Henry akapewa alichokihitaji huku akiwa ameshikilia kisu chake mkononi na baadae akampiga picha na Video msichana huyo kisha akizirusha mtandaoni na ku share na rafiki zake.

Polisi Wameshamkamata mwanaume huyo, ingawa amekana mashtaka hayo  yupo mahabusu kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana na kesi yake itasikilizwa tena tarehe 4 mwezi wa 9, 2013.

Wema Feki Atapeli watu Face Book, Angalia Ushahidi hapa na Kaa Chonjo


Katika kujihakikishia maisha kirahisi rahisi, wimbi la matapele limebuni mbinu mpya na kufungua Akaunti katika Mitandao ya Kijamii kupitia majina ya Watu Maarufu Kisha Kuwahusisha na Utapeli wao.

Kupitia Ujangili huo wameweza kuwatapeli mamia ya watumiaji wa mitandao hiyo hususan hapa kwetu Tanzania. Leo hii naomba niwatahadharishe Watanzania na watumiaji wa mitando ya kijamii hasa Face Book Kuhusu Uwepo wa Tapeli alijifungulia Akaunti ya Face Book na Kujiita Wema Abraham Sepetu, huku akiweka picha ya Mwanadada wema akiwa katika Kochi kama anavyoonekana hapo chini.


 Mbaya zaidi huwahusisha watu katika kutapeli bila kukusudia kwani Huwa Tag katika Page zao Akiandika Post zake za Kitapeli Hususani Kuhusu Hii Mikopo ya Kiwizi wizi kama Alingalia hapa MIKOPO YA KIWIZI WIZI YA WEMA SEPETU WA UONGO


Kwa Ushahidi wa Page ya Tapeli Huyo ni Hii Hapa WEMA WA UONGO NA TAPELI WA MIKOPO

Bongo Gossip Blog wala Face book page Haina Uhusiana na Tapeli Huyu na Kuanzia Sasa Tume Block Contact zake zote na Tunawatahadharisha Watanzania na Watumiaji wa Mitandao ya Kijamii Hasa Face Kuwa Makini zaidi na Kuchuku hatua Stahiki.

Najua Atabadilisha baada ya hili kugonga Mwamba na Atakuja na Jingine Tukae Chonjo.

Tafadhali Tuwe Makini. Akitapeliwa Mtu Tusilaumiwe Bure. Leo Tarehe 07/08/2013. Nawasilisha.


Rihhana Ajiachia Uch! katika Carnival Barbados, Angalia Picha Zote Hapa.


Aliyekuwa Mpenzi wa muda mrefu wa msanii Criss Brown, Rihanna Jumamosi hii aliamua kupunga mawazo na ku make headlines tena pale alipoamua kujiachia kihasara hasara alipokuwa katika Carnival Barbados kama anavyoonekana Pichani.

Pichani hapo juu ni jinsi gani Mzuka umempanda na ku bong'oa kabisa huku akizii kujiacha wazi. Kiafrica sijui tunalionaje hili? haya bwana ndo Ulaya Ulaya Tena.