Wema Feki Atapeli watu Face Book, Angalia Ushahidi hapa na Kaa Chonjo


Katika kujihakikishia maisha kirahisi rahisi, wimbi la matapele limebuni mbinu mpya na kufungua Akaunti katika Mitandao ya Kijamii kupitia majina ya Watu Maarufu Kisha Kuwahusisha na Utapeli wao.

Kupitia Ujangili huo wameweza kuwatapeli mamia ya watumiaji wa mitandao hiyo hususan hapa kwetu Tanzania. Leo hii naomba niwatahadharishe Watanzania na watumiaji wa mitando ya kijamii hasa Face Book Kuhusu Uwepo wa Tapeli alijifungulia Akaunti ya Face Book na Kujiita Wema Abraham Sepetu, huku akiweka picha ya Mwanadada wema akiwa katika Kochi kama anavyoonekana hapo chini.


 Mbaya zaidi huwahusisha watu katika kutapeli bila kukusudia kwani Huwa Tag katika Page zao Akiandika Post zake za Kitapeli Hususani Kuhusu Hii Mikopo ya Kiwizi wizi kama Alingalia hapa MIKOPO YA KIWIZI WIZI YA WEMA SEPETU WA UONGO


Kwa Ushahidi wa Page ya Tapeli Huyo ni Hii Hapa WEMA WA UONGO NA TAPELI WA MIKOPO

Bongo Gossip Blog wala Face book page Haina Uhusiana na Tapeli Huyu na Kuanzia Sasa Tume Block Contact zake zote na Tunawatahadharisha Watanzania na Watumiaji wa Mitandao ya Kijamii Hasa Face Kuwa Makini zaidi na Kuchuku hatua Stahiki.

Najua Atabadilisha baada ya hili kugonga Mwamba na Atakuja na Jingine Tukae Chonjo.

Tafadhali Tuwe Makini. Akitapeliwa Mtu Tusilaumiwe Bure. Leo Tarehe 07/08/2013. Nawasilisha.