Diamond Ahudhuria Mazishi ya Mzee Sepetu, Awapa Makavu waliomkusudia Mabaya.


Msanii Nassib Abdul maarufu kama Diamond Platnumz akiwa na kampan ya Zamaradi na Babu Tale waliweza kufunga safari mpaka Visiwani Zanzibar na kushiriki katika shughuli ya kumpuzisha Baba wa Muigizaji wa Bongo Movies, Wema Sepetu.

Mbali na kuhudhuria huko, Diamond ameacha Ujumbe katika Akaunti yake ya Instagram kwa baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema nae. Soma zaidi hapo chini.



 






Babu Tale, Zamardi na Diamond ndani ya Zanzibar kwaajili ya mazishi ya Balozi Sepetu 


Habari ndo hiyo kwa wazushi. Well done Prezident wa Wasafi na leo naona ametokelezea ki Al Haj zaidi.

Ufoo Saro Aelezea Tukio zima Lilivyokuwa.


MWANDISHI  wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye hivi karibuni alikumbwa na madhila ya kupigwa risasi na kujeruhiwa vibaya na mzazi mwenzie, ameanza kufunguka kidogo kidogo na kueleza kwa kina jinsi tukio zima lilivyotokea.  
Akizungumza kwa sauti ndogo na taratibu na gazeti hili kando ya kitanda alicholazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, mwanahabari huyo alieleza kushangazwa na ujasiri na nguvu za aina yake ambazo zilimwezesha kutambaa na kujiburuza hadi eneo la karibu ya barabara ili kuomba msaada wa kukimbizwa hospitali.

Ufoo ambaye alionyesha dhahiri kutofurahishwa na baadhi ya taarifa zinazozingira tukio lake, alisema tayari alikuwa amewahakikishia polisi waliofika kumjulia hali hospitalini hapo kwamba alikuwa akisubiri afya yake iimarike kabla hajaeleza kwa kina kila anachokijua kuhusiana na tukio hilo.

“Alifika hapa kunijulia hali na kuangalia maendeleo yangu afande Msangi na nikasema nitakuwa tayari kueleza kila ninachokijua baada ya afya yangu kuimarika. Nasikitika kuna watu wanasema mambo wakifikia hatua ya kutaka kuonekana wananifahamu vizuri kuliko hata ninavyojifahamu mwenyewe,” alisema akionyesha kutofurahishwa na baadhi ya taarifa zinazoripotiwa kuhusu sakata lake.


Ufoo ambaye alifikishwa hospitalini hapo Jumapili ya wiki iliyopita kutokana na kujeruhiwa kwa risasi na mwanaume aliyezaa naye mtoto mmoja alisema anamshukuru sana Mungu kwa uzima alionao sambamba na kuelezwa kupata faraja kubwa na kutiwa moyo na mwajiri wake, ndugu, jamaa na marafiki.

Mwanahabari huyo ambaye bado yuko chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuondoa risasi mwilini mwake siku chache zilizopita, amelazwa katika chumba cha peke yake ambacho ingawa kina seti ya televisheni alisema alikuwa haruhusiwi kuiangalia kwa ushauri na maelekezo ya madaktari.

Huku akionekana wa chini ya uangalizi mwingine wa karibu na wa kudumu wa muuguzi ambaye muda wote wa mazungumzo haya alionekana kuwapo katika chumba hicho, Ufoo alisema alikuwa ana mapenzi makubwa kwa mzazi mwenzake huyo ambaye alipoteza maisha katika tukio hilo.

“Nilimpenda sana Antheri. Alikuwa kijana mtaratibu na mpole sana. Najua kile kilichotokea ni shetani tu na binafsi nilishasamehe alfajiri ile ile baada ya tukio lile,” alieleza Ufoo ambaye pia alimpoteza mama yake mzazi katika mkasa huo.

TUKIO ZIMA LILIVYOTOKEA

Ufoo ambaye mara kadhaa katika mazungumzo na gazeti hili alionekana kukunja uso akiashiria kupata maumivu, alionyesha eneo la chini ya bega katika mkono wake wa kulia lililofungwa na bandeji ambalo alisema ndipo alipopigwa risasi ya kwanza wakati akigeuka na kujaribu kuepuka mauti muda mfupi baada ya Antheri kumfyatulia risasi zilizomkuta mama yake mzazi.

Akijaribu kuvuta kumbukumbu ya tukio lilivyoanza, Ufoo alisema mzazi mwenzake huyo alifika nyumbani kwake akitokea Sudan alikokuwa akifanya kazi usiku huo huo wa tukio na akamtaka kwenda kwa mama yake (Ufoo) eneo la Kibamba, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Kabla ya kufika Kibamba na kwa sababu ambazo Ufoo hakuzieleza, alimkariri mzazi mwenzake huyo akisema alikuwa amefikia uamuzi wa kujiua yeye na mtoto wao.

“Hata sijui ni nini kilitokea. Wakati tukitoka nyumbani Antheri alianza kwa kuniambia kwamba alikuwa amepanga kujiua yeye na mtoto wetu,” alisema Ufoo kabla ya kukaa kimya kwa sekunde kadhaa na kuendelea na simulizi yake ya kusikitisha.

Akiwa na sura ya ujasiri, Ufoo anasema pamoja na kumwambia maneno hayo bado Mushi alimsisitiza kwamba waende kwa mama yake (Ufoo) baadae warudi kumchukua mtoto wao japo Ufoo hakusema walitaka kwenda wapi baada ya hapo.

Alisema walipofika nyumbani kwa mama yake walikwenda moja kwa moja sebuleni na wakiwa wamekaa kwenye makochi baada ya salamu za hapa na pale ghafla Mushi akasimama akamwambia mama yake Ufoo kwamba; “Mama nimeishafanya maamuzi”

Kwa mujibu wa maelezo ya Ufoo, baada ya Mushi kutamka maneno hayo ghafla akaingiza mkono nyuma ya suruali  alikokuwa ameweka bastola  yake na kisha akaichomoa.

Katika maelezo yake Ufoo alisema baada ya kuichomoa bastola hiyo mama yake naye alisimama na kwenda kujaribu kumpokonya, kitendo hicho kilimfanya amiminiwe risasi mfululizo.

Alisema kuona hivyo aliamua kukimbia kuelekea jikoni ambapo Mushi alimuona na kuanza kumiminia risasi ambayo moja ilimpata eneo la mkono wa kulia ambayo ilitokezea mbele na kuchana titi la kulia.

Kwa mujibu wa Ufoo jeraha hilo halikumfanya akate tamaa ya kunusuru maisha yake kwani alijaribu kukimbia ingawa Antheri alifyatua risasi nyingine kadhaa ambazo zilimpata juu kidogo ya mgongo na kutokea tumboni ambazo zilisababisha aanguke chini

Akiendelea kusimulia, anasema ingawa alikuwa akivuja damu nyingi, na huku akijiburuza ardhini, Ufoo alisema wakati akitambaa aligeuka nyuma na akamuona Antheri akijielekeza bastola eneo la kidevu na alipofyatua risasi alianguka chini.

“Nikiwa chini nilimuona Antheri akijipiga risasi kidevuni na akaanguka chini, sikujua kilichofuata baada ya hapo kwani niliendelea kujiburuza ili kuokoa maisha yangu,” alisema Ufoo

ALIVYOJIOKOA

“Nyumbani kwetu, pale Kibamba si mbali sana na barabarani, wakati nikikaribia kufika barabarani wakati huo nikitokwa na damu nyingi huku nikihisi tumbo langu limejaa sana nilikutana na dada mmoja ambaye nilimuomba khanga ili nijifunge kuzuia damu zisitoke kwa wingi”.

Anasema dada yule alimpa khanga akajifunga na aliposogea barabarani alikutana na gari lililokuwa likiendeshwa na mwanamke mmoja.

“Nilipoona kuna gari linapita nikainuka kuomba msaada. Liliposimama nilimuona mwanamke akiendesha nikamweleza kwamba nilikuwa nimepigwa risasi na nilikuwa nikiomba msaada wake anikimbize hadi katika hospitali ya Tumbi na kwamba akifika pale tu aniache mlangoni.

“Si rahisi kuamini, yule mama alikataa kunisaidia akisema alikuwa akiwahi sehemu kumchukua mzazi. Sina la kusema niliamua kumsamehe tu yule mama ingawa niliumia sana,” alisema Ufoo.

Alisema muda mfupi tu baadaye alitokea kijana aliyekuwa na pikipiki, maarufu kwa jina la bodaboda ambaye alimuomba msaada wa kumkimbiza hospitali ya Tumbi na akakubali.

“Yule kijana aliniuliza iwapo nilikuwa ninao uwezo wa kujishikilia vizuri na niliposema nitaweza akanisaidia kupanda katika bodaboda.

“Wakati huo nilikuwa naona kama tumbo linazidi kujaa. Nikiwa kwenye pikipiki kuna wakati nilikuwa nikihisi kwamba naweza nikaishiwa nguvu na kuanguka katika barabara na kisha kupitiwa na gari na kupoteza maisha. Lakini nilipata ujasiri na kujishikilia,” alieleza kwa sauti ya chini.

Alisema anakumbuka wakati walipofika eneo la Kibaha ilipo mizani ya kupima uzito wa magari makubwa walikuta barabara ikiwa imejaa magari na yeye alimuomba dereva huyo wa bodaboda kupita hata nje ya barabara eneo la nyasi ili kumwahisha hospitalini jambo ambalo kijana yule alilifanya.

“Nilipofika eneo la mapokezi pale Tumbi nilimueleza muuguzi niliyemkuta kwamba nilikuwa nimejeruhiwa kwa risasi na nikamuomba asaidie kuokoa maisha yangu. Yule nesi alisita akitaka kwanza kupata kibali cha polisi (PF3) lakini nikaumuomba apigiwe simu, Kaimu Mganga Mkuu wa Tumbi, Dk. Dattan ambaye tunafahamiana”

“Baada ya muda mfupi Dk. Dattan alifika na nikamweleza yaliyonipata na mara moja nikaanza kuhudumiwa kwa kuniwekea dripu, na nikamsikia akiwaeleza wauguzi kwamba isingekuwa busara kwa hali niliyonayo kama wangeanza kuchukua picha za X-ray kwani hatua hizo zingeweza kusababisha kupoteza maisha,” alieleza akikumbuka yaliyojiri hapo Tumbi.

Kwa mujibu wa Ufoo, akiwa bado ana fahamu alimsikia daktari aliyekuwa akimhudumia akiomba msaada wa gari la kubeba wagonjwa ili limchukue na kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wito ambao ulijibiwa kwa maelezo kwamba lilikuwa halina mafuta.

Majibu hayo kwa mujibu wa Ufoo, yalisababisha daktari huyo aombe kuletewa gari la wagonjwa la wagonjwa maarufu (VIP) ambalo lililitwa na muda mfupi baadaye akapakizwa tayari kwa safari ya kukimbizwa Muhimbili.

Alisema wakati akikimbizwa Muhimbili anakumbuka namna alivyokuwa akipatwa na maumivu makali wakati wote gari ile ya wagonjwa ilipokuwa ikipanda matuta ya barabarani na kuna nyakati alikuwa akihisi kupoteza pumzi na kuishiwa nguvu. 
 

MTANZANIA

Chris Brown matatani kwa shambulizi kwenye hoteli ya nyota tano mjini Washington DC



Na MOblog Team kwa msaada wa mtandao
Mwanamuziki maarufu nchini Marekani Chris Brown yu matatani tena kwa kufanya shambulizi la mwilini kwa kumpiga ngumi na kumsukuma mmoja wa wageni katika moja ya Hoteli ya hadhi ya nyota tano jijini Washington, DC majira ya asubuhi ya 4.30 na kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kwenye moja ya kituo cha Polisi jijini huo.
Tukio hilo limefanyika jijini Washington, DC na limesababisha mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kukamatwa kwa shambulio hilo.
kwa mujibu wa sheria za Marekani, mtu akifanya kosa la kumshambulia mwenzake anaweza kwenda jela kwa miaka minne, Brown gwiji la muziki wa R’n'B ambaye alipewa kifungo cha nje kama msamaha  kwa kosa kama hilo kwa kumshambulia mpenzi wake wa zamani Rihanna  mwaka 2009. 
article-2477846-1906CECC00000578-806_634x372 
Gari za Polisi likiwa limezingira basi la Chris Brown (Tour Bus) analotumia kwenye safari zake za muziki likiwa nje ya Hoteli aliyolala jijini Washington DC.
Brown na walinzi wake wote wamekamatwa kwa mahojiano zaidi baada ya mwanamuziki huyo kumshambulia mmoja wa wageni katika hoteli hiyo ya nyota tano jijini Washington D.C.
kwa kawaida Chris na mpenzi wake Rihanna huwa wana tabia ya kugombana baada ya matumizi ya madawa ya kulevya lakini siku hiyo Rihanna  hakuwa katika ushawishi wa madawa ya kulevya au pombe.
Mabishano yalitokea katika kulizunguka gari la Brown baada ya walinzi wake kutaka kugomea amri ya polisi ya kumkamata mapema jioni ya siku ya tukio  lakini baadaye alipelekwa kituo cha polisi chini ya ulinzi mkali. Mwathirika wa tukio hilo alivunjika pua na kupelekwa hospitali kwa matibabu.
Chanzo cha habari kinasema sababu hasa ya Brown kumpiga mtu huyo akijajulikana mara moja

Kengete Blog.

Mke na Hawara Wachomwa Moto Hadi Kufa Baada ya Kufumwa na Mume wakisaliti Ndoa yao.



Wawili hao ambao kiumri ni sawa na mama na mtoto wake, waliteketea kwa moto baada ya nyumba waliyokuwa wamelala kuchomwa moto na mtu aliyetajwa kwa jina la Zacharia Mwingila (39) mkazi wa Tunduma wilayani Momba.
Chanzo cha mauaji hayo kimetajwa kuwa ni wivu wa kimapenzi ambapo mtuhumiwa ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi alifikia hatua ya kuchoma moto nyumba baada ya kumkuta mpenzi wake akiwa amelala na Wasiwasi majira ya saa tano za usiku wa Oktoba 25, mwaka huu katika Kijiji cha Magamba wilayani Chunya.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo,  walisema mtuhumiwa huyo alianza kwa kuwachoma na visu wagoni wake na ndipo alipoamua kuchoma moto nyumba nzima ambayo iliwateketeza hadi kufa.
Kaimu kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Robert Mayala alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuisihi jamii kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mikononi.

Gesti Bubu Nyingine Inayofuga Machangudoa Yabainika


MZEE mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Abdullahimu Mnami (48) amenaswa akiendesha gesti bubu kinyume cha sheria za nchi.

Baadhi ya wananchi walionaswa katika msako wa biashara haramu ya ukahaba. Pichani ni wauzaji na wanunuzi.
Tukio hilo lilitokea Oktoba 26, mwaka huu maeneo ya Tuangoma jijini Dar, baada ya waandishi wetu kuzinyaka taarifa hizo na kuzifikisha kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo, Chande Mohammed aliyefika eneo hilo na polisi.
Awali, ili kujiridhisha, mmoja wa mapaparazi wetu alijifanya mteja na kufika katika gesti bubu hiyo, kisha kupangisha chumba kwa malazi ya siku moja kwa malipo ya shilingi 3000 tu lakini pasipo kuandikisha mahali popote.
Mmiliki wa gesti bubu inayotumika katika biashara haramu ya ukahaba baada ya kutiwa nguvuni.
Akizungumza na waandishi wetu mbele ya maaskari na mwenyekiti, mzee huyo alisema alishindwa kuisajili gesti yake kwa kuwa haikuwa na viwango vinavyokubalika na manispaa (ya Temeke).
“Ningefuata utaratibu, manispaa isingeniruhusu kutokana na ubora wa vyumba vyenyewe, kama mnavyoona. Pia njaa tu jamani ndiyo imenifanya nianzishe gesti hii,” alisema mzee Abdullahim.
Eneo la ndani ya gesti bubu inayotumika kwa ukahaba.
Hata hivyo mwenyekiti wa mtaa huo, alisema kuwa mzee huyo ana kesi ya kujibu kwa kukiuka taratibu za kibiashara zilizowekwa na halmashauri na kumuamuru aifunge gesti hiyo mara moja huku akiahidi kumpeleka Baraza la Kata kwa ajili ya masikilizano ya awali.
Timu yetu iliwaachia msala wao na kuendelea na oparesheni nyingine ambapo walifanikiwa kuwanasa machungudoa wakijiuza jirani na mtaa huo huku ikielezwa kuwa, wateja wa madadapoa hao hupelekwa katika gesti bubu ya mzee huyo kwa vile ni bei poa.
Wateja na wafanyabiashara haramu ya ukahaba wakiwa chini ya ulinzi baada ya kunaswa.
GPL

Rose Ndauka anamuamini Hubby aliompa ujauzito wake


STAA wa sinema za Bongo, Rose Ndauka amesema suala la kubeba mimba ya mpenzi wake, Malick Bandawe kabla ya ndoa halikutokea bila mpangilio, walishauriana kabla.
Rose Ndauka akiwa na mpenzi wake, Malick Bandawe.
Akipiga stori na paparazi wetu, Rose alisema hajutii kubeba mimba hiyo ambayo ameitangaza kwa vile alishauriana na mwandani wake huyo na anamuamini.
“Sijajibebea tu mimba hovyohovyo hata Malick alipogundua hali hii alifurahi sana, ndiyo maana sina presha hata kidogo kwa kuwa sisi ni wapenzi wa muda mrefu na tunaaminiana,” alisema Rose.

GPL.

Instragram Wamfungia Akaunti Maheeda, ni baada ya Kuzidi kuweka Picha za Uch* na Ngon*





Yule mwanamke anaeongoza kwa kuweka picha za Utup* na za Ngon* kutoka nchini Nigeria ambaye awali alikuwa anajiuza, akasalimika na kuokoka na baadae akarudi tena katika mabo yake ya biashara ya Ngon*, Maheeda jana alifanya kali kuliko zote baada ya Kuweka picha ya mmoja wa wateja wake akipiga Punyet0 huku uum3 wake ukionekana na akiwa ameshikilia picha Maheeda akiwa Uch wa Mnyama.

 Kufuatia Tukio Hilo Kampuni inayomiliki mtandao wa Instagram Umeifunga Akaunti ya Muuza Sukari Huyo, Amesema anafikiria kuhamia YouTube.

Karrueche Tran aweka picha hii Instagram kumuumiza Rihanna



Wapenzi wanaogombana na kutengana kila mara wamerudiana tena huku mwanadada Karrueche Tran akisistiza kwamba yeye na Criss Brown watakuwa pamoja milele daima.

D,banj naye Aleta Mapenz* Stejini na Mnenguaji wake, Angalia Video Hapa


Katika Finali za mwaka 2003 za Kumuenzi Mwanamuziki Fela, D'Banj naye aliamua kupagawisha kwa staili yake baada ya kupanda stejini akiwa kama Bondia flani na kuanza kucheza Kingon* ngon* Stejini na Mnenguaji wake.

Angalia Video Hapa Chini

"Usanii Unalipa, Range Rover Nimenua kwa Pesa yangu " Irine Uwoya


Baada ya mashabiki  wengi kuanza  kumponda mwanadada Irene Uwoya kuwa gari aina ya Range Rover aliyoinunua amehongwa na washika dau, mwanadada huyo ameibuka na  kusema kuwa mali anazomiliki amezinunua kwa pesa zake anazopata kwenye uigizaji  pamoja na zile zinazotokana na biashara zake nyingine.

 “Kwa nini watu hawataki kukubali kuwa kazi ya uigizaji inalipa, yaani sisi tukinunua magari tumehongwa? Yaani wa kuhongwa ni sisi tu na si tasnia nyingine?” alihoji Uwoya.

Aidha Uwoya alisema kuwa kazi ya filamu ukijua kuitumia vizuri kwa kujiwekea malengo na kuitumia vizuri kila senti unayoipata, unaweza kupata mafanikio makubwa.

“Tunaigiza sehemu nyingine ambazo hutaki hata mwanao aone, hii siyo kazi rahisi maana yake ni kwamba kama ukiipatia unaweza kujikuta unaingiza pesa kila siku kwani mwaka mzima uko kazini,” alisema

Irene amesema kuwa ameamua kuweka wazi ukweli huo kutokana na maneno yaliyozagaa kuwa magari anayomiliki amenunuliwa na wanaume wanaomweka mjini.

Source: Bongomovies



Angalia Video ya yule mganga aliyekamatwa na kiganja cha binadamu huko Mwanza




Watu watatu wakiwemo waganga wawili wa jadi wamekamatwa na polisi katika eneo la Igombe Tx, jijini Mwanza wakiwa na kiganja cha mkono wa kulia unaoaminika kuwa wa binadamu.


Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, kamishna msaidizi wa polisi Joseph Konyo amesema tukio hilo limetokea eneo la kati ya ziwani na nyuma ya uwanja wa ndege wa Mwanza baada ya raia wema kuwapa taarifa za siri.

 ANGALIA VIDEO HAPO CHINI:-



Mshindi wa " SURA MBAYA" Zimbabwe, achekelea mafanikio yake


William Masvinhu kwa mara nyingine tena amenyakua taji la Mwenye Sura Mbaya huko Zimbabwe katika shindano lililofanyika siku ya Ijumaa ndani ya ukumbi wa City Sports Bar.

Amepewa taji, hela pamoja na Ofa ya mwanae mmoja kulipiwa ada ya shule kwa mwaka mmoja, mke wake William naye alikuwepo ukumbuni hapo na alifurahia sana ushindi huo wa mumewe.

Katika kujifaharisha na taji lake, William alisema" Ubaya wa Sura yangu ni wa Asili, ingawa nilijiaanda kidogo kwa shindano hili lakini mengine niliyaacha yajishughulikie yenyewe"

Photo: William Masvinhu won the title of the ugliest man in Harare
Hao ndio washiriki wote kwa ujumla ambapo William alitoka Kidedea.

Ahadi za Mwanaume wake ni 'Kitandani tu" akimaliza anasahau kila kitu.


Habari hii nimeikuta sehemu, nami nimeileta huku, Analalamika Mwanada huyu ambaye yuko katika mahusiano ya Kimapenz na Mwanaume wake kwa zaidi ya mwaka sasa, kinachompa wakati mgumu ni tabia ya mpenz wake huyo kutoa ahadi kibao hasa za kumuoa pindi wanapokuwa "Faragha" lakini akishamaliza haja zake jamaa anasahau ahadi zote.

Kwa upande wake, mwanamke anashindwa la kufanya huku akiwa anaona aibu na kuhofia itakuwaje mwanaume huyo akikasirika na kumuacha, hivyo anaomba ushauri nini afanye.


WANAUME WAMENILA URODA BURE MIAKA MINGI SANA BILA FAIDA SASA HIVI SIRUDII KOSA NG'OO: ANTI LULU!


Katika mahojiano yake na gazeti moja hapa jijini nimesikia aunt lulu akisema wanaume wamemla sana uroda bure kwa miaka mingi sana bila faida, ila kwa sasa harudii kosa hilo ni mwendo wa faranga kwa kwenda mbele, sincerely kwa hizo pics hapo juu nani anaweza akawa na mwanamke kama huyu and shower her dollazzzz?? men also haaaaa as they say one man's meat is another man's poison.

 kwahio tusiliongelee sana ila wakati mwingine maneno tunayaongea ktk media yanafanya wasanii waonekane kituko katika jamii kabisa na akili zako na unajitambua wewe ni msanii  unaweza ukaongea pumbaless kama hii na watu wakasoma na kukuelewa ??


hiki ni nini wajameni? nikisema mtasema Sintah anaongea?? niko hapa kwaajili ya kurekebisha watu na jamii inachukulia wasanii kama kioo chao, sasa kwa matendo haya ya lulu na alivyoongea wengine tunaonekana vipi,  ni wakati umefika sasa tujue kuna wasanii na wanaotafuta umaarufu ili ya kwao yawaendee eg kupata mabwana na wanawake   yaani nimekereka sana na hii kauli ya Aunt Lulu so sasa hivi anauza rasmi na ameamua kujitangaza kama tunavyojua biashara ni matangazo ?? God  forbid. i do the seeking n u do the judging...

Alisema Sintah.

Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitoa pole kwa mjane na Familia ya Balozi Isaac Sepetu


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole mjane wa Balozi Isaac Sepetu, Mama Miriam Sepetu, alipokwenda na Mama Salma nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam, kutoa pole kwa mjane huyo na familia ya Marehemu Sepetu aliyefariki jana jijini Dar es salaam.
w6
w2
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa pole kwa wanafamilia wa Balozi Isaac Sepetu alipokwenda na Mama Salma nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam, kutoa pole kufuatia msiba Marehemu Sepetu aliyefariki jana  jijini Dar es salaam.
w3
Mke wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akimfariji mjane wa Balozi Isaac Sepetu alipokwenda  nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam, kutoa pole kufuatia msiba Marehemu Sepetu aliyefariki juzi  jijini Dar es salaam
w4
Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa Balozi Isaac Sepetu  alipokwenda  nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam, kutoa pole. Marehemu Sepetu aliyefariki juzi  jijini Dar es salaam.
w5
Mama Salma Kikwete  akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa Balozi Isaac Sepetu  nyumbani kwa marehemu Sinza Mori, Dar es salaam. .

Azam Wamlamba Mnyama 2-1, Wakaa kileleni mwa Ligi.


Timu ya Soka ya Azam FC Jana imefanikiwa kuiondoa Simba katika usukani wa Ligi Kuu soka Tanzania bara baada ya kuichapa goli 2-1 katika mchezo wa 11 wa timu hizo kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara. magoli ya Azam yalifungwa na Kipre Chetche  huku la Simba likifungwa na Ramadhan Singano 'Messi'.

COASTAL Union ya Tanga imezinduka baada ya sare na vipigo vilivyofuatana,nayo ikiifunga Mtibwa Sugar ya Morogoro mabao 3-0 Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
 Coastal ambayo sasa iko chini ya makocha wa muda, wachezaji wake wa zamani, beki Joseph Lazaro na mshambuliaji Razack Yussuf ‘Careca’ ilipata mabao yake leo kupitia kwa viungo Wakenya Crispin Odula dakika ya 20, Jerry Santo 38 kwa penalti na mshambuliaji mzawa, Danny Lyanga dakika ya 88.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo, Ruvu Shooting imetoka sare ya 1-1 na Kagera Sugar ya Bukoba, Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.
Kagera Sugar ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa mpachika mabao wake mahiri, Themi Felix dakika ya 36 na Said Dilunga akaisawazishia Ruvu dakika ya 72.
Kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha, wenyeji JKT Oljoro wamelazimishwa sare ya bila kufungana wa ‘Watoto wa Jiji’, Ashanti United ya Ilala, Dar es Salaam.










MSIMAMO WALIGI
 Pos.LogoClubPWDLGFGAGDPts
1Azam FC116501771023
2Simba SC1155121101120
3Mbeya City FC10550137620
4Young Africans SC1054121111019
5Mtibwa Sugar FC104421611516
6Ruvu Shooting Stars114431310316
7Kagera Sugar FC114431210216
8Coastal Union SC1026265112
9JKT Ruvu Stars10406911-212
10Ashanti United112451018-810
11Tanzania Prisons10154613-78
12Rhino Rangers10145815-77
13JKT Oljoro FC11146716-97
14JKT Mgambo10127318-155