ANGALIA PICHA 5 ZA WANAFUNZI WA HOSTELI WAKIJIACHIA BAADA YA KUWA MBALI NA WAZAZI WAO



Wazazi, ni vyema kwenu kujijengea mazoea na utaratibu wa kuwa karibu na watoto wenu hasa linapokuja suala la mahusiano yao na marafiki.

Inawezekana kabisa kuharibikwa kwa mwanao kukatokana na aina ya watu anaokuwa nao karibu, kitu ambacho naamini kama mzazi usingependa kitokee kwa mwanao.
 
Utajisikiaje ukikuta aina hii ya picha ya ndugu yako....?


BINTI WA MIAKA 17 ANASWA AKIJIUZA KATIKA GESTI BUBU


KIKOSI kazi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ Kanda ya Ziwa, kinaendelea kufukua uchafu unaofanyika jijini hapa, safari hii kimemnasa binti mwenye umri chini ya miaka 18 akifanya ukahaba wikiendi iliyopita bila wasiwasi wowote.
Anitha baada ya kunasa katika mtego wa OFM.
OFM Kanda ya Ziwa, kikiwa ni kitengo kipya kilichoteuliwa rasmi kushughulikia kadhia za mikoa yote inayozunguka Ziwa Victoria kilinasa tukio hili laivu na kulifuatilia kwa kina ili kutoa ukweli kamili kwa jamii.
HABARI KAMILI
Timu yetu ilishuhudia binti huyo akiwa amechanganyikana na mabinti wengine wakubwa wakijiuza kwa wateja wa baa mbalimbali katika eneo la Mabatini jijini hapa huku wakitumia gesti bubu iliyopo maeneo hayo.
Kwa siku tatu mfululizo, mapapazari wetu walimfuatilia na kujionea namna binti huyo mdogo akichukuliwa na mababa watu wazima na kwenda kula nao uroda kwa nyakati tofauti.
Anitha akivaa nguo zake baada ya kunaswa akifanya ukahaba.
AINGIA MTEGONI
Ili kupata ushahidi wa tukio hilo, makamanda wetu waliingia mzigoni na mmoja wao akajifanya mteja ambapo alimtokea binti hiyo ambaye alikubali kwenda kulala naye  kwa dau la shilingi 5,000.
Binti huyo aliyejitambulisha kwa jina la Anitha aliongozana na kamanda wetu hadi ndani ya gesti bubu inayotumika kwa uchafu huo bila kujua kwamba alikuwa ameingia ‘choo cha kiume’.
Anitha akiohojiwa baada ya kunaswa akiwa kazini.
OFM KAZINI
OFM wakiwa na wadau wengine waliokubali kushiriki katika zoezi hilo ambalo ni aibu kwa uongozi wa jiji hili na serikali kwa jumla, walikuwa tayaritayari jirani na gesti  hiyo wakisubiri maelekezo kutoka kwa kamanda aliyeingia na changudoa huyo mtoto.
Vifaa vya mawasiliano vya OFM vilifanya kazi yake vyema ambapo kamanda aliyekuwa chumbani alitoa maelekezo kwa wenzake kuwa changudoa yule, alikuwa amesaula ndipo wakaingia na kufotoa picha za kutosha.
MSIKIE MWENYEWE
Alipogundua kuwa kumbe ulikuwa mtego wa kumnasa aliomba asamehewe kwa madai kwamba alilazimika kufanya vile kwa lengo la kujitafutia maisha kwa vile kwao hali ni mbaya.
Anitha akiwa mikononi mwa wanausalama.
“Jamani mimi ni mdogo, nina miaka 17, sina baba wala mama na hali ya maisha ni ngumu ndiyo maana niliamua kuingia kwenye biashara hii,” alisema Anitha.
Hata hivyo, uchunguzi wa Risasi Mchanganyiko, umeonyesha kuwa, Anitha ni muongo kwani ametoroka nyumbani kwao Mahina, Nyakato ambako alikuwa akiishi na wazazi wake na kukatisha masomo yake akiwa kidato cha pili.
Chumba alipokutwa Anitha kitandani pakiwa na kinga.



WAZAZI SOMENI HAPA
OFM inatoa wito kwa wazazi kuwa makini na malezi ya watoto wao kwa kuwafuatilia mara kwa mara ili wasiharibike na kuiga tabia kama ya Anitha. Aidha, wazazi wa Anitha wanapaswa kuchukua hatua za makusudi kumwondoa binti yao katika biashara hiyo mbaya inayohatarisha usalama wa afya yake.

MCHEKI ETOO AKIWA NA MWANAE HAPA



Cheki picha zake alipokuwa mdogo uwanjani na akicheza kabumbu.


Samuel na David baada ya Fainali ya Copa De Rey
Baba na Mwana mnamo 2007

MCHEKI ETOO AKIWA NA MWANAE HAPA



Cheki picha zake alipokuwa mdogo uwanjani na akicheza kabumbu.


Samuel na David baada ya Fainali ya Copa De Rey
Baba na Mwana mnamo 2007

AFANDE AACHA LINDO BENKI NA KWENDA KUMKAMATA DEREVA WA BODABODA


Afande akiwa amemdhibiti dereva wa bodaboda.
Wasamaria wema wakijaribu kumbembeleza afande.
Afande akiwa…
Afande akiwa amemdhibiti dereva wa bodaboda.
Wasamaria wema wakijaribu kumbembeleza afande.
Afande akiwa amecharuka hataki kusikia cha mtu.
Afande kakomaa.



Afande aliyekuwa akilinda Benki ya NMB iliyopo Mtaa wa Samora karibu na Idara ya Habari 'Maelezo' jijini Dar, leo mchana aliacha lindo lake na kuanza kukamata bodaboda zilizokuwa zikivunja sheria za usalama barabarani kama anavyoonekana pichani akimdhibiti mwendesha bodaboda.

ABIRIA 213 WANUSURIKA KIFO BAADA YA NDEGE YAO KUTUA KWA DHARULA KATIKA UWANJA MDOGO WA ARUSHA


Abiria 213 waliokuwa wakisafiri na ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia jana walinusurika kifo baada ya ndege hiyo kutua kwa dharura katika uwanja mdogo wa Arusha.
Ndege hiyo aina ya Boeing 767, ilitua saa 6.45 mchana katika uwanja huo baada ya kushindwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) kutokana na kupata pancha kwa ndege nyingine inayomilikiwa Shirika la Ndege la Tanganyika (TFC), kwenye njia ya uwanja huo.

Ndege ya Ethiopia ililazimika kuelekea Arusha na kutua kwenye uwanja huo mdogo kuweza kupokea ndege kubwa kutokana na kuishiwa mafuta.
Ndege hiyo iliyokuwa inatokea Addis Ababa, Ethiopia ikiwa pia na wahudumu 23, baada ya kutua kwenye Uwanja wa Arusha, ilinasa kwenye tope baada ya tairi lake la mbele kuvuka sehemu ambayo lami inaishia kutokana na ufupi wa njia zinazotumiwa na ndege zinapotua kwenye uwanja huo.
Jitihada za kuiondoa ndege hiyo zilishindikana jana. Ndege hiyo ilikuwa ikielekea Johannesburg, Afrika Kusini kwa kupitia Kia na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema: “Rubani amejitahidi kutua katika uwanja huu japo ni mdogo ili kuokoa maisha ya abiria kwani walikuwa hawana mafuta ya kutosha kwenda uwanja mwingine.”
Tukio la ndege hiyo kutua kwa dharura limekuja siku chache tangu ndege ya Shirika la Ndege la Precision iliyokuwa na abiria 37 kupasuka matairi manne ilipokuwa ikitua kwenye Uwanja wa KIA Jumamosi 

BIFU LA HEMED NA YUSUPH MLELA LAZIDI KUPAA



Hemed (kushoto) akimtishia bastola Mlela
Hemed na Mlela wakiwa wamelazwa hospitalini baada ya kuumizana huku mama yao akiwaangalia kwa huzuni…
Ni katika Filamu yao Mpya ya I KNOW YOU.

BILIONEA AKUTWA AMEFARIKI NDANI YA GARI DAR, ASEMEKANA KAJIUA MWENYEWE


NI jambo lililotoa mshtuko kwa Jeshi la Polisi Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani ambapo Desemba 10, mwaka huu, walikuta mwili wa binadamu ukiwa ndani ya gari lililopinduka, pembeni mwa Barabara ya Kisarawe - Mwaneromango.

Mbali na mwili, ndani ya gari hilo aina ya Toyota RAV 4 (milango mitatu new model) lenye namba za usajili T 273 AKP kulikutwa bastola moja, risasi 85 na magazini mbili.

Utata ukaanzia hapo, polisi wa wilaya hiyo wakiongozwa na mkuu wao (aliomba jina lisitiriwe kwa sababu si msemaji) wakajiuliza ni nani mtu huyo ambaye alikuwa amefariki dunia? Kumbe alikuwa Suleiman Muhema (42), bilionea kijana mkazi wa jijini Dar es Salaam.

polisi waliuchukua mwili wake na kwenda kuuhifadhi katika Hospitali ya Wilaya mpaka ndugu walipokwenda kuuchukua kwa mazishi.

SULEIMAN MUHEMA NI NANI?
Suleiman Muhema ni mkazi wa jijini Dar, amejenga jumba la kifahari Kijitonyama ambako aliishi na mke wake, Zihji Mvungi (42).

Mpaka kifo chake alikuwa mfanyabiashara wa magari kutoka Japan akiyauza Dar, pia alikuwa na kampuni ya usafirishaji, sifa zote kwa pamoja zinamfanya aitwe bilionea.

MAISHA SIKU CHACHE KABLA YA KIFO
Habari zinadai kuwa, marehemu alikuwa ndani ya mgogoro wa kifedha na mtu ambaye hakutajwa jina lakini ni wa karibu naye.
Inadaiwa kuwa, mgogoro huo ni wa muda mrefu na ulikuwa ukisuluhishwa na Dawati la Jinsia, Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar.

SIKU YA TUKIO
Siku ya tukio inadaiwa marehemu alikuwa Magomeni na watu (idadi yao haikujulikana). Baada ya hapo aliondoka  kwenda kusikojulikana lakini baadaye alimpigia  simu ndugu wa karibu na kumwambia kuwa yuko mahali (hakupataja) ametekwa na sauti anayoitoa inaweza kuwa ya mwisho kisha akakata simu.

MAELEZO YA POLISI SASA
Kwa mujibu wa chanzo chetu ndani ya Jeshi la Polisi Wilaya ya Kisarawe, Desemba 10, mwaka huu,  usiku wa saa nane,  marehemu alionekana akiwa ndani ya gari jeusi umbali wa kilomita saba kutoka Kisarawe Mjini lakini aliondoka baada ya kuliona gari la ‘patroo’ ya polisi.

Chanzo hicho kikasema kuwa dakika chache mbele polisi waliokuwa katika shughuli za ulinzi usiku huo waliliona gari hilo likienda pembezoni mwa barabara na kupinduka.

“Tulilifuatilia, tukalikuta limepinduka, ndani ya gari tulimkuta mtu amekufa kwa kujipiga risasi kwani sehemu ya kidevuni na kwenye utosi kulikuwa na tundu la risasi,” kilisema chanzo hicho.

MAREHEMU ALIDHANIWA MHALIFU
Habari zinasema katika upekuzi wa awali ambapo polisi walimkuta marehemu akiwa na bastola, risasi 85 na  magazini mbili walidhani alikuwa mhalifu aliyetaka kutekeleza uhalifu mahali ndani ya walaya hiyo.

NDUGU WA MAREHEMU WANA NENO
Kwa upande wao ndugu wa marehemu ambao waliomba majina yao yawekwe pembeni, walisema kuna mkanganyiko mkubwa kuhusu kifo cha ndugu yao huyo kwa sababu hata kifo chake hawakielewielewi.
Akizungumza kwa hisia ya uchungu, ndugu mmoja alisema katika maisha ya jijini Dar, yeye ndiye baba wa marehemu lakini hakuna alichojua toka kifo hadi kuzikwa.

Alisema hata mazishi ya marehemu alishtukizwa  kwamba anazikwa siku hiyo jambo lililompa wakati mgumu kufikiria.
 “Sisi kama ndugu wa marehemu, tulipenda akazikwe nyumbani, Makete   (Njombe), lakini ghafla tukaambiwa anazikwa hapahapa Dar tena siku hiyohiyo tuliyopewa taarifa,” alisema ndugu huyo.

MKE WA MAREHEMU NAYE
Kwa upande wake mke wa marehemu Zihji alipoulizwa na mapaparazi wetu juzi kuhusu sakata la kifo cha mumewe alijibu kuwa kila mtu anaweza kuongea jambo lolote.

Aliongeza kusema anachojua yeye ni kwamba kifo cha mumewe kilitokea kama ambavyo mtu mwingine angeweza kufa.

KAMANDA WA POLISI ANASEMAJE?
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, ACP Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa marehemu alikutwa akiwa na jeraha la risasi moja hali ambayo ilionesha alijipiga risasi mwenyewe pengine kutokana na mambo yaliyokuwa yakimsonga kichwani.

BILIONEA AZIKWA DAR
Marehemu Muhema alizikwa Desemba 11, mwaka huu kwenye Makaburi ya Sinza jijini Dar. Ameacha mke na watoto watatu wa kike. Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.

MASWALI TATA
Kifo cha Muhema kina maswali tata mengi. Kwanza, kama kweli alipanga kujiua kwanini alikwenda mbali na Jiji la Dar es Salaam?

Pili, kwa nini damu ndani ya gari ilikuwa kidogo wakati uzoefu unaonesha kuwa, mtu anayepigwa risasi ndani ya gari huacha damu nyingi?

Tatu, ndugu mmoja wa marehemu alikiri kuwa, Muhema alinunua bastola mwaka huu ili kujilinda, sawa kabisa. Je, kwa nini akutwe na risasi nyingi kiasi hicho kama alikuwa anakwenda kufanya uhalifu?

Nne, ilidaiwa alimpigia simu ndugu mmoja akidai ametekwa na huenda asisikike tena. Polisi walikuta simu kwenye gari lake, kwa nini waseme alijipiga risasi mwenyewe?

GPL

PICHA ZA MATUKIO KATIKA UZINDUZI WA AZAM TV


Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Yusuf Bakhresa (kushoto) akifungua rasmi Azam Tv  mbele ya Mtendaji Mkuu wa Azam Media Rhys Torrington.
Mmoja wa watoa huduma kwa wateja akiwa tayari kuwahudumia wateja.…
Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Yusuf Bakhresa (kushoto) akifungua rasmi Azam Tv  mbele ya Mtendaji Mkuu wa Azam Media Rhys Torrington.
Mmoja wa watoa huduma kwa wateja akiwa tayari kuwahudumia wateja.
Kutoka kushoto ni Maulid Kitenge,  Mhariri Kiongozi wa Magazeti ya Championi Saleh Ally na mmoja wa wafanyakazi wa Azam Tv.
Keki maalum zenye jina la Azam Tv kwa ajili ya wadau.
Kikundi cha burudani cha ngoma za asili kikitoa burudani kabla ya ufunguzi.
Wateja wakipata huduma muda mfupi baada ya ufunguzi.



Wasanii mbalimbali wa Filamu nchini nao walikuwepo kwenye shamrashamra hizo za ufunguzi wa Azam Tv.

YOUNG DEE AKAUNUSHA KUHUSU SKENDO YA KUFUMANIWA NA LULU WAKILA RAHA ZA UKUBWANI NDANI YA GARI



Juzi kupitia kwenye kipindi cha U-heard cha Clouds FM chini ya bwana Sudi Brown ama Gossip Cop kulikuwa na fununu kali iliyokuwa inamuhusu mwanadada wa Bongo Movies na mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya Young D 'Young Dar es Salaam' kama mwenyewe anavyojiita baada ya wawili hao kukutwa kwenye gari wakifanya lile tendo linaloruhusiwa kufanywa mara baada ya mdada na mkaka kufunga ndoa.
Young D
                                                                                              

Kwa mujibu wa Sudi Brown 'Gossip Cop' wawili hao walikutwa maeneo ya Mbezi Beach ndani ya gari aina ya Hyundai ya mwanadada Lulu na polisi wa doria wakivunja amri hiyo iliyokatazwa na vitabu vyote vitakatifu kwa maana ya biblia, Quran na vitabu vingine vya dini ulimwenguni.

Habari zainasema baada ya wawili hao kukutwa eneo hilo na polisi walipelekwa pembeni gizani na kuongea na Polisi kabla ya wao kutokomea wasipojulikana na gari hilo.

Alipopigiwa simu mwanadada LULU alipokea na kukata muda mfupi na baadaye Young D alipopigiwa simu alitoa majiu ya utata kama alivyoongea mwenyewe kupitia kwenye kipindi cha U-heard cha Clouds Fm.
GPL

ABAKWA, ANYONGWA HADI KUFA NA KISHA KUINGIZWA CHUPA SEHEMU ZA SIRI HUKO CHALINZE




JAMANI jamani! Dunia imefika pabaya zaidi, Mungu asaidie. Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga, inauma sana kwa kweli!
  Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga.
Tukio hilo la kutisha lilijiri usiku wa Desemba 7, mwaka huu Chalinze Kwamwarabu ambapo mwanamke huyo alikwenda kujumuika na ndugu na majirani katika mkesha wa ngoma ya kuwatoa wari siku ya Jumapili.
                                                              Eneo la tukio Chalinze Kwamwarabu.
Mkasa huu unasimuliwa kwa majonzi mazito na mdogo wa marehemu ambaye alikuwa mshehereshaji wa shughuli hiyo ‘MC’, Siwema Rashid.
Alisema: “Mpaka sasa tunashindwa kuelewa kilichotokea maana siku ya tukio tulikuwa naye kwenye ngoma usiku. Alikuwa mchangamfu sana, aliifanya shughuli ipendeze.
“Ilipofika saa nane usiku baadhi ya watu walianza kulala, sasa sijui yeye ilikuwaje mpaka hali hiyo ikamfika maana hao watu walichomfanyia wametuachia historia kubwa sana.
“Walimbaka wakaona haitoshi wakamwingiza chupa ya soda sehemu ya siri ya mbele halafu wakamwingiza chupa ya bia sehemu ya siri ya nyuma.
“Ili kuzidi kutimiza unyama wao, waliondoka na kumwacha kama alivyozaliwa, inauma sana halafu matukio ya hivyo yamekithiri sana.”
Aliongeza: “Marehemu ametuachia jukumu la malezi kwa watoto wake wawili, Sikudhani Juma (18) na Ally Juma (12).”
Naye mtoto mkubwa wa marehemu, Sikudhani akisimulia kifo cha mama yake, alisema: “Nasikitika sikuweza kuuona mwili wa mama hata pale watu walipojazana na kumshangaa.
“Hata polisi na mganga mkuu wa mkoa walipofika kumchomoa zile chupa sikutaka kusogea kabisa, naamini Mungu atawaonesha jambo hao watu hapahapa duniani.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Yurichi Mtei akizungumzia ukatili huo alisema: “Taarifa za tukio hilo bado hazijafika kwangu kutokana na majukumu mengine ya kikazi, isipokuwa nalifanyia kazi kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa.”
Tukio hilo lilifunguliwa jalada kwenye Kituo cha Polisi Chalinze kwa nambaCH/RB/3767/2013 MAUAJI.
Mpaka kifo chake, mwanamke huyo alikuwa akiishi na mwanaume mmoja (jina halikupatikana mara moja lakini si aliyezaa naye watoto hao wawili). Alizikwa Jumapili iliyofuata, Chalinze.
Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.

GPL

BAADA YA MIAKA 112, BARAFU YAANGUKA NA KUJAA CAIRO


Watu wengi wanapolifikiri jiji la Cairo hakika watakuwa wanafikiria juu ya mazingira ya joto na vumbi.

Ila kitu kimoja kisichokuwa cha kawaidia kimetokea kwenye eneo hilo usiku - barafu imemwagika.


Kwa mujibu wa waandishi wa ndani wamesema hii ni mara ya kwanza kwa barafu kushuka kwenye mji huo mkuu wa Misri ndani ya miaka 112.

Picha za kushangaza zimeonyesha mji huo ambao mara nyingi huwa ni wenye joto ukiwa umefunikwa na weupe wa barafu.

Wananchi wa Misri walitumia mtandao wa Twitter kuposti baadhi ya picha za hali hiyo ya kushangaza.




DC Blog.