Raia Wawili wa Uingereza Wamwagiwa Tindikali Zanzibar.

Majeruhi wa Tindikali, Si wa Habari Hii
Raia wa kigeni kutoka katika nchi ya Uingereza ambao wanafanya kazi ya kujitolea katika upande wa Ualim   wamemwagiwa tindi kali mjini Zanzibar jana  mida ya saa moja usiku katika mitaa ya shangani mji mkongwe  Zanzibar habari kutoka katika chanzo chetu cha habari  kinasema jeshi la polisi zanzibar limeanza msako na kuwatafuta watu waliofanya kitendo hicho.

  walimu hao ambao wamefika mjini Zanzibar kwa kujitolea kufundisha walitambulika kwa majina ya Kate Gee miaka 18 na kirsiwer Trup pia miaka 18 walimu hao wa kujitolea wanatoka katika nchi ya Uingereza (UK)  raia hao wameingia kisiwani hapo takribani wiki mbili tu na kukutwa na majanga hayo ambao walikuwa wanafanya kazi katika shule  moja ya msingi inayojulikana kama Mtakatifu Monika iliyopo chini ya kanisa la Aglicana. habari tulizozipata hivi punde  Raia hao hivi sasa wamehamishiwa katika Hospitali ya Aghakani jijini Dar es salaam kwa matibabu zaid tutazidi kuwaleta habari zaidi

From: Swahilitz